Friday, August 10, 2012

GLOBAL PUBLISHERS YAZINDUA SHINDANO LA ‘SHINDA NOAH’


Abdallah Mrisho akionyesha mojawapo ya simu aina ya Samsung Galaxy ambazo zitashindaniwa sambamba na Noah hiyo.Kushoto ni Mhariri Kiongozi wa Magazeti ya Championi, Saleh Ally na kulia ni Flugence Isakefu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano huo wa uzinduzi, Meneja Mkuu wa Global, Abdallah Mrisho, amesema huo ni utaratibu ambao kampuni imejiwekea kurudisha sehemu ya mapato kwa wateja wake na kama ilivyokuwa kwa miaka mitano iliyopita, mwaka huu gari aina ya Noah litatolewa.

“Mbali na zawadi hiyo ya gari, zawadi nyingine ambazo ni simu za mkononi, televisheni, na nyingine kibao zitatolewa kwa wasomaji wa magazeti pendwa na kwa kutuma kuponi kwa anuani elekezi,” alisema Mrisho.

Mgeni rasmi katika promosheni hiyo inayoanza mwezi huu wa Agosti na ambayo itafikia kikomo mwezi Novemba, alikuwa ni Ofisa Tarafa wa Magomeni, Flugence Isakefu, ambaye alifika kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Lugimbana.
Isakefu akifungua mlango wa gari aina ya Noah linaloshindaniwa.
...Akizindua shindano hilo.
Gari aina ya Noah linaloshindaniwa.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...