Tuesday, August 28, 2012

CHADEMA YATEMBEZA BAKULI KUCHANGIA WAFIWA, MAJERUHI VURUGU ZA POLISI MORO

 
KATIBU mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Wilbroad, Slaa jana
 alilazimika kuendesha shughuli ya kuomba msaada wa fedha kutoka kwa watu waliofurika kwenye mkutano wa chama hicho mjini Morogoro ili kuwachangia wafiwa na walioathirika na vurugu zilizoanzishwa na polisi dhidi ya wafuasi wa chama hicho.
Akifafanua, alisema zitatumika kuwasaidia majeruhi wawili waliopigwa risasi na polisi jana ambao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro.
Pia fedha hizo zitapekwa kwa familia ya marehemu Ally Zolla anayesemekana aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi wakati wa vurugu hizo.
Mmiongoni mwa watu waliozunguka na bakuli hilo ni pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika.
Fedha hizo hazikufahamika idadi yake hadi mwandishi wetu anaondoka kwenye viwanja hivyo majira ya saa moja usiku.

Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika akichangisha michango hiyo.
Michango iliyopatikana ikihesabiwa na makamanda.


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...