Wednesday, August 15, 2012

ALICHOKIFANYA RAIS MUSEVEN KWA MGANDA ALIESHINDA OLYMPIC.





.

Baada ya kurudi home, Maelfu ya waganda wamempokea Stephen Kiprotich mshindi wa medali ya dhahabu kwenye riadha ya Olympic 2012 ambapo ameifanya Uganda itangazwe mshindi wa medali hiyo baada ya miaka 40.

Kiprotich ambae ni askari magereza alieshinda kwenye mbio za wanaume jumapili iliyopita ndani ya Olypic 2012, amezawadiwa cheki ya dola za kimarekani elfu 80 ambazo zimetolewa na Rais Yoweri Museveni ambae pia amempandisha cheo mara tisa kwenye kazi yake ya uaskari Magereza.

Standard Media wameripoti kwamba mzigo ulikua mzito manake watu walipanga foleni kumpokea Stephen huko Entebbe akiwa amebebwa kwenye gari ambalo lilikua na plate namba iliyoandikwa UG GOLD.


Hii ndio nyumba aliyokua akiishi Stephen.

Watu walikua wengi mpaka waliziba njia ambapo magari yaliyokua kwenye msafara yalikosa pa kupita wakati yakielekea ikulukumpeleka Stephen kunywa chai asubuhi na Rais Museveni.

Baada ya Kiprotich kupewa cheki yake ya dola elfu 80, alimuomba rais Museveni kuwajengea wazazi wake nyumba kaskazini mashariki mwa Uganda ambapo rais Museveni amekubali kujenga hiyo nyumba ya vyumba vitatu.

Kwenye line nyingine ni kwamba rais Museven ameahidi kwamba katika muda ujao, mwanamichezo yoyote wa Uganda atakaeshinda medali ya kimataifa, atakua analipwa shilingi shilingi milioni moja za Uganda kila mwezi.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...