Monday, May 7, 2012

USIKU WA MASHAUZI CLASIC WATIKISA DAR LIVE

Mashabiki wakicheza mduara ulioporomoshwa na Chuchu Sound.
MASHABIKI waliofurika katika uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live huko Mbagala, jijini Dar es Salaam, jana Jumapili waliburudika kwa muziki kabambe kutoka kwa wataalam wa muziki wa bendi za Chuchu Sound, Twanga Pepeta, Mashauzi Classic na muziki wa kizazi kipya wa Afande Sele. Furaha hiyo ilikwenda sambamba na furaha ya wapenzi wa timu ya soka ya Simba ambao walikuwa na furaha wa kuwafunga wapinzani wao Yanga kwa magoli 5 -0.

Shabiki akipuliza vuvuzela wakati wa burudani hizo. Isha Mashauzi akiimba na Afande Sele.

Afande Sele akikamua.

Wanamuziki wa Chuchu Sound Joniko Frawa (kushoto), H. Mbizo na Mao Santiago wakiimba kwa pamoja. Baadhi ya mabaunsa wakiangalia usalama wa mashabiki ukumbini hapo. Mau Santiago wa Chuchu Sound akifanya vitu vyake.Isha Mashauzi akiimba wimbo wake wa ‘Mama Nipe Radhi’. Wanamuziki wa Twanga Pepeta wakisubiri zamu yao jukwaani.




No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...