Wednesday, April 11, 2012

MAREHEMU STEVEN KANUMBA AZIKWA MAKABURI YA KINONDONI KWA HESHIMA KUBWA, KWELI ALIKUWA MTU WA WATU

Waombolezaji wa msiba wa Marehemu Steven Charles Kanumba wakishusha jeneza lenye mwili wa marehemu kwenye kaburi, tayari kwa kumpumuzisha katika nyumba ya milele kwenye makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo jioni , Kanumba atakumbukwa kwa kazi yake nzuri katika tasnia ya filamu hapa nchini, ambapo alijitangaza na kuitangaza nchi vyema ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania kupitia filamu zake nyingi alizoigiza.
(MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMEN)
Mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba Bi. Flora Mgoa na ndugu wa karibu wakiaga mwili wa marehemu kwa mara ya mwisho makaburini Kinondoni.
Waombolezaji wakitayarisha jeneza la marehemu Steven Kanumba tayari kwa kuliweka kaburini.
Mmoja wa waombolezaji akibebwa baada ya kupoteza fahamu makaburini.
Wajenzi wa kaburi la marehemu wakichanganya Sementi kwa ajili ya kufukia.

Mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba Bi. Flora Mgoa akiuaga mwili wa mwanaye kwa mara ya mwisho kabla ya kuzikwa rasmi katika makaburi ya Kinondoni.
Wafanyakazi wa msalaba mwekundu wamefanya kazi ya ziada kutoa huduma ya kwanza kwa waombolezaji
Polisi wakiweka ulizi wa kutosha katika mazishi hayo.

Mwanamitindo maarufu mtanzania anayefanya kazi zake za mitindo nchini Marekani Millen Magese akienda kuweka shada la Maua kwenye kaburi la marehemu Steven Kanumba.
Mama wa Marehemu Steven Kanumba akiweka shada la maua mkaburini

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...