Tuesday, January 31, 2012

VODACOM YATANGAZA PROMOSHENI YA PUNGUZO LA GHARAMA
· *Wateja kupiga simu kwa robo shilingi na Kutuma SMS kwa Sh. 25/-

Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imetangaza promosheni ya aina yake ya punguzo la gharama za simu kupiga na kutuma ujumbe mfupi wa maneno- SMS itakayowahusisha wateja wa kampuni hiyo ambao sasa watapiga simu kwa gharama ya ROBO SHILINGI kwa sekunde.


Promosheni hiyo ya siku saba kuanzia Jumatatu Januari 30, 2012 inahusu kupiga simu za ndani ya mtandao wa Vodacom yaani kupiga Vodacom kwenda Vodacom kati ya Saa nne usiku na saa moja asubuhi kila siku kwa wateja wote wa malipo ya kabla

Aidha sanjari na ofa hiyo kamambe Vodacom imetoa pia punguzo la gharama ya kutuma ujumbe mfupi wa maneno hadi shilingi 25/- kwa ujumbe wakati wote wa siku kwenda mtandao wowote wa simu ya mkononi nchini kwa kipindi cha siku saba nayo pia kuanzia leo Jumatau Januari 30, 2012.

Akitangaza promosheni hizo mbili Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Bw. Rene Meza amesema ni imani yake kwamba katika kipindi chote cha siku saba cha promosheni hiyo wateja watafurahia kwa kufanikishiwa mawasiliano ya biashara, familia, kazi na mengineyo kwa gharama nafuu zaidi.

“Wateja wa Vodacom wakati wote wanafurahia huduma bora, nzuri na zenye kukidhi mahitaji halisi, ni wazi kipindi hiki cha siku saba cha promosheni hii ya punguzo la gharama za upigaji wa simu na utumaji SMS kitawapatia wakati mwengine bora wa kufurahia kuwa wateja wa kampuni inayoongoza soko”Alisema Bw. Rene.

Promosoheni hii inakwenda sawa na azma ya Vodacom ya kutoa fursa ya watanzania kuunganishwa kimawasiliano na kubadili maisha.

Ili mteja wa Vodacom aweze kufurahia promoheni hii ya punguzo la gharama za mawasiliano anapaswa kwanza kujiunga kwa kupiga *100# na kuanzia hapo atakuwa na uwezo wa kufurahia mawasiliano nafuu zaidi nchini miongoni mwa mitandaso ya simu za mkononi.

“Ni fursa nzuri kwa wateja wetu, tunawaomba waitumie ikiwa ya kiwango cha chini zaidi kuwahi kutokea katika soko la mawasiliano ya simu za mkononi nchini na Vodacom itaendeleza utamaduni wa kuwa kinara wa kubuni na kuleta sokoni promosheni pamoja na huduma zenye thamani na mantiki halisi ya wateja wetu na jamii nzima nchini.” Aliongeza Bw. Rene

Rene aliongeza kwa kusema “Tunapoangalia katika utaratibu wetu wa kawaida wa mfumo wa maisha tanagundua kuwa muda wa kati ya saa nne usiku na saa moja asubuhi ndio wanafamilia hukaa pamoja na kufanya mawasiliano yenye lengo la kupashana habari za familia na hata kazi na biashara baada ya majukumu ya kutwa nzima au kabla ya kuanza siku mpya, hivyo ni imani yetu tumewapa wateja kitu chenye thamani na kinachoweza kutumika vema na kumnufaisha kila mteja.”Aliongeza

Vodacom ikiwa na wateja zadi ya milioni kumi nchini ni wazi promosheni ya aina hii itatoa faida kubwa kwa jamii kwa kuwawezesha kutumia sehemu ya punguzo la gharama ambazo wangengia kupiga na kutuma ujumbe mfupi wa maneno kuelekeza sasa fungu hilo katika matumizi ya mahitaji mengine

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...