Sunday, January 29, 2012

MECHI KATI YA WATANGAZAJI WA RADIO NA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI LAFANA KATIKA VIWANJA VYA TTCL- KIJITONYAMA.
Siku iliyokuwa inasubiriwa na Watanzania kuhusiana na mechi kali kati ya Watangazaji, mapromota na waimbaji wa nyimbo za injili waliotegemea kupambana na wacheza filamu (Bongo Movie). Zoezi hili  halikuweza kufanikiwa kutokana timu ya Bongo Movie kuwa na mualiko Zanzibar katika tamasha lao la ZIFF. Badala yake kamati iliamua kupambanisha kati ya Waimbaji wa nyimbo za injili na Watangazaji wa radio za kikriso Tanzania. 

Tamasha lilionekana kuvutiwa na Watanzania wengi. Timu ya Watangazaji ilipigwa bao 2 na Waimbaji kuibuka washindi kwa mabao 5. Mfungaji bora wa watangazaji alikuwa Mtangazaji wa Channel Ten ambaye alikuwa mtangazaji wa radio ya  Praise Power, Boniface Magupa aliyefunga mabao mawili na kujipatia Tsh. 5000 kama mfungaji bora.

Mbali na mashindano ya mpira ya miguu kulikuwa na mchezo wa kufukuza kuku ambapo Mwimbaji wa Glorious Celebration, Jessica Honore alijishindia kuku na upande wa watangazaji wa radio, Yusuf Magupa wa Praise Power alishinda na kujipatia kitoeo cha kuku.

Waimbaji kama Martha Mwaipaja, Martha Ramadhan, Glorious Celebration na wengine wengi walionekana kugusa mioyo ya watu kwa  nyimbo zao zenye kumwinua Mungu wetu.

 Baadhi wa wachezaji wakiwa katika kiwanja cha shule ya Kenton Sinza wakijiandaa kuelekea katika uwanja wa Posta-Kijitonyama.
Stori zikiendelea.....

 Timu ya waimbaji ikiwa katika kiwanja cha mazoezi Kenton Sinza
 Timu ya Watangazaji ikiwa katika kiwanja cha mazoezi Shule ya Kenton, Sinza

WACHEZAJI WAKIWA KATIKA UWANJA WA POSTA KIJITONYAMA
Bony Mwaitege (aliyevalia jessy nyeupe) akiufuatilia mpira
Goolkeeper wa watangazaji kutoka radio ya Praise Power, DP akiwa ameshikilia bori baad ya kufungwa.


MC  Uncle Jimmy

 Kipindi cha kujitambulisha


 Mashabiki
 Mtangazaji Kisaka



 Kipindi cha mapumziko



 Timu ya Waimbaji katika kipindi cha mapumziko







 Msikilizaji maarufu wa Praise Power a.k.a Mzee wa Kubonya
 Mtangazaji wa Praise Power (kulia), Uncle Jimmy na Mchekeshaji Chavala (kushoto)

 Mzee wa mblogu na mawebsite pamoja na mgarphics, Rulea Sanga (katikati akiwa amezungukwa na waimbaji wa Glorious Celebration
Mtangazaji wa Wapo Radio, Silas Mbise (kulia) akiwa na rafiki zake. Kutoka kushoto ni Jessica na lilian
Watangazaji wa mpira wakiwa katika corner yao
 Waimbakji wa Glorious Celebration wakitoa huduma yao ya juimbaji katika pambalo la mpira



Glorious Celebration Live Band
Mwimbaji wa Glorious Celebration, Jessica Honore (anayepunga mkono), akiwaongoza waimbaji wenzake baada ya kushuka jukwani


Martha Mwaipaja

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...