Sunday, October 18, 2015

Baadhi ya wachezaji wa Simba SC, wakishangilia goli lao baada ya kuichapa Mbeya City.

SIMBA Sports Club ya jijini Dar es Salaam, jana imevunja mwiko wa kufungwa na kutoa droo na timu ya Mbeya City baada ya kuwafunga goli moja kwa sifuri katika dimba la Sokoine, ushindi ambao ni historia kwao kutokana na kuteswa na wanakomakumwanya hao kwa mda wa misimu miwili iliyopita.

Histori ya wagonga nyundo  imevunjwa na  Simba kwa goli moja tu maridadi lililowekwa nyavuni na Mganda wa timu hiyo Juuko Murushidi dakika ya pili ya mchezo, goli ambalo katika ligi kuu msmu huu litakuwa la  mapema zaidi katika uwanja huu ukiachia mbal goli la Atupele Green wa Ndanda FC,  liliofungwa dakika ya 3.

Kikosi cha Simba SC, na Mbeya City kikipambana kabla ya Juuko kupachika bao.
Wachezaji wa Simba SC, Mussa Hassani Mgosi na Juuko Murushidi wakishangilia baada ya kuifunga Mbeya City.

Staili ya ushangiliaji ya ina yake iliyoonyeshwa na wachezaji wa Simba.
..wakishangilia kwa pamoja.
Mabosi wa timu ya Simba wakifurahia jambo uwanjani hapo.
Mmoja wa mashabiki wa  Mbeya City akiwa amebebwa kwenye machela baada ya kupoteza fahamu kwenye mchezo huo.



TASWIRA KATIKA PICHA ZA MAPOKEZI YA DIAMOND PLATNUMZ DAR ES SALAAM





















Wednesday, October 14, 2015

ZIZZOU FASHION YAWAPA VIFAA VYA MICHEZO CHANGANYIKENI RANGERS

Mkurugenzi wa Duka la Zizzou Fashion, Athumani Tippo (kushoto), akimkabidhi vifaa vya michezo kocha wa timu ya Changanyikeni Rangers, Steven Nyenge ndani ya duka hilo lililopo maeneo ya Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam.

DUKA la vifaa vya michezo la Zizzou Fashion mapema leo lilijitolea kutoa msaada wa vifaa vya michezo kwa timu ya soka ya Changanyikeni Rangers inayoshiriki Ligi Daraja la Pili.
Akizungumza katika makabidhiano hayo Mkurugenzi Zizzou Fashion, Athumani Tippo alisema kwamba, amelazimika kutoa mchango wake kwa timu hiyo kutokana na kuonyesha juhudi, uwezo na kujituma kwa wachezaji wa timu hiyo kwa muda mfupi tangu ilipoanzishwa.

“Niameamua kutoa mchango wangu wa vifaa vya michezo kwa timu hiyo kwani imenishawishi baada ya kuifuatilia kwa muda sasa ambapo nimeziona juhudi za kocha wao, Steven Nyenge na wachezaji wote kwa ujumla wanavyojituma kuhakikisha wanapanda daraja,” alisema Tippo.
Tippo akiwa katika pozi na kocha wa timu ya Changanyikeni Rangers (katikati), na Kocha wa timu ya watoto ya Boko Beach Veterani, Maswanywa
 MOSHI VETERANI YAWACHAKAZA BOKO

Kikosi cha timu ya Boko Beach Veterani kikiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya mchezo huo kuanza.
 TIMU ya wakongwe ya Moshi Veterani Wikiendi iliyopita iliitembezea kichapo Boko Beach Veterani kwa bao 1-0 kwenye mechi ya kudumisha urafiki baina ya timu hizo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Boko jijini Dar es Salaam.
Nahodha  Moshi Veterani, Jafari Kiango (kushoto), akimkabidhi mchezaji wa timu ya Boko, Godfrey Malekano ‘Messi’,  zawadi ya Mchezaji Bora wa Mwezi kwa niaba ya Zizzou Fashion, muda mfupi baada ya kumalizika kwa mchezo huo.

DANSA WA DIAMOND AIBEBA TIMU YA MPIRA MTAANI KWAO

 Mcheza shoo wa Diamond (wa tatu kutoka kulia nyuma), Dumy Utamu akiwa kwenye pozi la pamoja na vijana wanaochezea timu ya mtaani kwao inayokwenda kwa jina la Young Boyz.


Monday, October 5, 2015

IDD AZAN AITEKA KINONDONI

2
Idd Azan (katikati), akikatiza Mitaa ya Mkwajuni wakati akielekea kwenye mkutano wake wa kampeni  uliofanyika katika Kata ya Hananasifu, jana jioni.
3
Azan akiteta jambo na Hassan Dalali, mjumbe wa CCM, Kata ya Hananasifu.
45
Hassan Dalali akimkaribisha Azan kwenye kikao cha kampeni muda mfupi baada ya kuwasili mahali hapo.
6
Kikundi cha ‘kudansi’ kikitoa burudani mahali hapo.
7
Azan akinadi sera zake jukwaani  kwa wakazi wa Kata ya Hananasifu, Kinondoni jijini Dar es Salaam, jana jioni.
89,
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan (katikati), akiwa amempakata mtoto aliyejitokeza na wazazi wake kusikiliza sera.
10
Mmoja wa wazee wa Kata ya Hananasifu akizungumza jambo na Azan baada ya kukutana naye njiani alipokuwa akielekea kwenye mkutano.
MGOMBEA wa kiti cha ubunge Jimbo la Kinondoni  kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),  Idd Azan jana aliwateka baadhi ya wakazi wa jimbo hilo waishio katika kata ya Hananasifu baada ya kukatiza kwa miguu wakati wa jioni alipokuwa akienda kwenye mkutano wa kampeni na baadhi ya wakazi wa kata hiyo kujitokeza kwa wingi na kuandamana naye hadi mahali mkutano ulipokuwa ukifanyikia.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 10:30 jioni ambapo Azan aliamua kutembea kwa miguu akitokea makao makuu ya ofisi za chama hicho zilizopo Kinondoni Mkwajuni jijini Dar es Salaam.
Habari/Picha: Musa Mateja/GPL

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...