AMA
kweli Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mama Kijacho,
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, sasa ni wa kimataifa zaidi ambapo
wakati mwanamama huyo akijiandaa kujifungua, tayari mtoto ajaye
ameandaliwa chumba maalum cha kulala na gharama za kumuona kwa
atakayehitaji picha hasa za kwenye vyombo vya habari, itakuwa si chini
ya Sh. milioni 20.
CHANZO KUTOKA WCB
Kwa mujibu wa chanzo makini
ambacho kipo ndani ya Wasafi Classic Baby (WBC), Diamond na Zari
wameamua kutenga chumba maalum cha mtoto wao atakapozaliwa.
MASHARTI YA KUMWAGA
Ilidaiwa kwamba, chumba
hicho kitakuwa mahususi kwa mtoto tu na wala hakuna mtu mwingine atakaye
ruhusiwa kuingia kumuona bila malipo zaidi ya mama, baba na familia yao
ambao nao wataingia kwa sharti la kutopiga picha.
“Naona Zari
anampeleka Diamond kimataifa kila kukicha maana nimeshuhudia chumba kina
‘full’ mazagazaga ya mtoto na nilipouliza nikaambiwa hicho ni chumba
cha mtoto wa Zari mara tu atakapozaliwa.
“Wanasema mtoto atakuwa na chumba chake maalum na hataruhusiwa mtu mwingine kulala wala kumuona.
“Kwa watu wa media (vyombo vya habari) lazima watoe si chini ya milioni 20 kwa picha na interview (mahojiano) na Zari.
KAMA KANYE NA KIM
“Wameamua kufanya hivyo ili
kuendana na wasanii wengine wa Marekani kama Kanye West na Kim
Kardashian au Jay Z na Beyonce ambao wamekuwa wakifanya hivyo.
ULINZI USIPIME
“Nimeshuhudia hadi vitu vya mtoto
na kitanda chake tayari vimeshaandaliwa mara tu mtoto atakapokuja
atakuwa katika chumba hicho ambacho kipo ndani ya mjengo wao, Madale
(Tegeta, Dar). Unaambiwa ulinzi utakuwa mkali usipime.
“Wamejipanga
mtu yeyote asimuone mtoto huyo kuanzia siku anajifungua kwani
wanategemea kuweka ulinzi wa hali ya juu kuanzia hospitalini hivyo hata
wanahabari wakihitaji lolote juu ya mtoto huyo watatakiwa kulipa kiasi
hicho cha fedha,” kilitiririka chanzo hicho.
BABA KIJACHO ANASEMAJE?
Baada ya kunyetishiwa
mchongo huo, gazeti hili lilimtafuta Baba Kijacho, Diamond ili
kuthibitisha ishu hiyo ambapo alisema ni kweli wameshaandaa chumba
maalum kwa ajili yake, mara tu atakapozaliwa na kwamba haitaonekana sura
yake kwani kutakuwa na bei maalum kwa yoyote atakayehitaji kumuona.
“Yeah! Ni kweli kuna chumba chake maalum na pia haitaonekana sura
yake maana kutakuwa na bei maalum kwa magazine au televisheni
itakayohitaji kuwa na ‘exclusive’ ya kuonesha sura yake kwa mara ya
kwanza.
“Bei ya mtu kumuona au kwa vyombo vya habari, hiyo
itategemea na ukaribu wetu na chombo husika kitakachokuwa kikihitaji
kurusha habari ya mtoto wetu,” alisema Diamond anayesumbua na kibao
chake kipya cha Nana.
DIAMOND PRESHA TUPU
Diamond kwa sasa yupo kwenye
presha kubwa ya kuomba mashabiki wake wampigie kura kwa wingi katika
Tuzo za MTV (Mama’s) baada ya kuteuliwa kuwania Vipengele vya Msanii
Bora wa Kiume Afrika, Mtumbuizaji Bora wa Kiume Afrika na Nyimbo Bora ya
Kushirikiana Afrika.
ZARI ATAJIFUNGUA LINI?
Kwa upande wake, Zari anatarajiwa kujifungua mtoto wa kike kuanzia Agosti, mwaka huu na kuendelea.
No comments:
Post a Comment