Mtangazaji na mwanamitindo, Karrueche Tran.
New York,MarekaniMTANGAZAJI na mwanamitindo, Karrueche Tran amemchana mpenzi wake wa zamani, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ katika mitandao ya kijamii.
Karrueche Tran akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Christopher Maurice ‘Chris Brown’.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Karrueche alimfungukia Chris kuwa
asimfuatefuate kwani mapenzi yao yalishakwisha tangu alipogundua kuwa
amezaa na mwanamke mwingine.“@chrisbrownofficial ulifanya mahojiano na Ryan Seacrest na ukaniongelea na ndiyo maana hata nilipofanyiwa mahojiano na Access Hollywood niliulizwa kuhusu wewe na nilijibu kama mtu aliyepevuka.“Niliongelea maisha yangu. Sikukuongelea. Usiwe mpumbavu wakati unajua uhusiano wetu ulikosa uaminifu.”
No comments:
Post a Comment