SAA chache kabla ya kuanza
kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, staa wa sinema za Kibongo,
Haji Adam ‘Baba Haji’ ameangusha bonge la harusi baada kufunga ndoa na
mrembo aliyetajwa kwa jina la Latifa Sharji wiki moja iliyopita huku
mastaa wakifanya kufuru kama kawaida yao.
Kabla ya pati hiyo iliyochukua nafasi kwenye Ukumbi wa Escape One
uliopo Mikocheni, Dar usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita, Baba Haji
alifunga ndoa na Latifa katika Msikiti wa Bungoni, Ilala jijini Dar.
Katika pati hiyo iliyohudhuriwa na mastaa kibao wa Bongo Movies huku
gazeti hili nalo likijipenyeza ndani, waalikwa walikula na kunywa hadi
wakasaza kabla ya muda wa zawadi na kusakata muziki.Kwenye shughuli
hiyo, kadiri watu walivyokuwa wakipiga ulabu ndivyo sherehe ilivyokuwa
ikichangamka na mastaa kujikuta wakiserebuka muziki kwa kwenda mbele.
Muda wa kutunza ulipowadia ndipo mastaa walipoanza kushindana kuwamwagia wanandoa hao ‘minoti ya wekundu wa msimbazi’.
Baadhi ya wasanii walioongoza kutunza ni tajiri mfupi, Steven Mengere
‘Steve Nyerere’ ambaye alimwaga fedha taslimu Sh. milioni 2 akifuatiwa
na Single Mtambalike ‘Richie’, Jacob Steven ‘JB’, Vincent Kigosi ‘Ray’
na wengine waliokuwa fedha za kudunduliza.
Kwa upande wa mastaa wa kike, Kajala Masanja ‘Kay’ aliongoza kwa
kumwaga mkwanja akifuatiwa na Jacqueline Wolper Massawe, Wastara Juma,
Jennifer Kyaka ‘Odama’, Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’ na watoto
wengine wa mjini.
Muda
wa kuserebuka ulipofika ilikuwa ni balaa tupu kwani Wolper aliweka
shida chini, akatupa mikono kule na kumwaga mauno hadi akajikuta
akimwaga ‘lazi’.
Hadi gazeti hili linaanua jamvi ukumbini hapo usiku mnene, baadhi ya
mastaa walikuwa wakiendelea kusakata rhumba na kupiga kinywaji.
No comments:
Post a Comment