Saturday, June 13, 2015

BEN POL, LINEX WAKINUKISHA BATA DAY

Msanii wa Bongo Fleva Ben Pol akikinukisha mbele ya mashabiki waliojitokeza kwenye Tamasha la Bata Day katika Ufukwe wa Azura.
Mmoja wa mashabiki akimnong’oneza jambo Ben Pol wakati shoo hiyo ikiendelea.
Linex akionyesha ubora wake katika jukwaa ambapo alikuwa akitumbuiza kwa kupigiwa vyombo laivu.
Linex akiimba na mashabiki wake.
Mtangazaji wa Radio Clouds FM, Adam Mchovu akiserebuka na mrembo jukwaani hapo.
Baadhi ya mashabiki wakicheza kwa pamoja baada ya kunogewa na burudani zilizokuwa zikiendelea ndani ya fukwe hizo.
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika shoo hiyo wakifuatilia burudani hizo kwa makini.
WASANII wa Bongo fleva wanaoimba kwa kucharaza magitaa laivu, Bernald Paul  ‘Ben Pol’ na Sunday Mangu ‘Linex’  wamefanya shoo kali usiku wa leo, ndani ya Fukwe za Azura, Kawe jijini Dar.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...