ALIYEKUWA Mkurugenzi
wa kundi la muziki la Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, Ali Chocky, ameamua kurudi
katika bendi yake ya zamani ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ inayomilikiwa na
Asha Baraka ambaye ni mkurungezi wa bendi hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari katika Hoteli ya Nemax Royal, kiongozi wa Twanga Pepeta,
Luiza Mbutu, amesema kurudi kwa wakongwe
na waasisi kwenye bendi yao ambao ni Chocky na Super Nyamwela, kutaleta nguvu
mpya na mapinduzi katika muziki wa dansi nchini kutokana na uwezo wao binafsi.
Kwa upande
wake, Chocky amesema kuamua kwake kurudi
katika bendi yake ya zamani ni kutokana na mapenzi yake binafsi na wala
hajalazimishwa na mtu huku akisisitiza kuwa hajafulia na ndiyo kwanza moto
umeanza.
“Tupunguze maneno-maneno;
kurudi kwangu na Super Nyamwela ndani ya Twanga si kitu cha ajabu, tumeamua
wenyewe na kila mtu ana uhuru wake binafsi wa kufanya jambo kwa muda muafaka
bila kupangiwa.
“Wakati
nasafiri kwenda Japan niliwaambia wanamuziki wa bendi yangu kwamba yeyote
anayeweza kunisubiri anisubiri na kama wapo watakaotaka kuondoka waende, lakini
niliporudi niliwakuta wameshatawanyika, sasa nipo nyumbani. Mashabiki wangu wategemee makubwa kutoka kwangu
kwani muda si mrefu nitaanza kupakua nyimbo kama vile Kichwa Chini, Usiogope
Maisha na nyingine nyingi,” alisema Chocky.
No comments:
Post a Comment