Monday, February 9, 2015

NDEMLA IS BACK, OWINO AJA KIVINGINE SIMBA CHEKI PICHA ZA MAZOEZI YA LEO JESHINI


Nimerudi... Kiungo staa, Ndemla akipiga tizi la pekee leo katika mazoezi ya kikosi hicho kinachojiandaa na mchezo dhidi ya Polisi Moro, Jumamosi, wiki hii.
Nyota aliye kunako kiwango cha kimataifa, Said Hamis Ndemla ameanza rasmi mazoezi na timu hiyo, baada ya kuwa nje akisumbuliwa na jeraha. Katika mazoezi ya kikosi hicho yaliyofanyika leo kwenye Uwanja wa Jeshi wa Mbweni, nje kidogo ya jiji kinda huyo alipewa programu maalum ya kufanya mazoezi ya peke yake akiwa chini ya uwangalizi wa daktari, Yassin Gembe.



Naye nahodha wa zamani wa klabu hiyo, Joseph Owino amezidi kuonekana fiti baada ya kufanya mavituzi ya ukweli katika mazoezi ya leo na kuonekana kupona kabisa.
Ancle is back... Joseph Owino (wa pili kulia) amezidi kuonyesha kiwango kizuri baada ya kupona majeraha yaliyokuwa yakimsumbua.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...