Saturday, February 7, 2015

DR CONGO YAICHEZESHA ‘BOLINGO’ GUINES IKWETA



Timu ya DR Congo imefanikiwa kushika nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Mataifa Afrika Afcon 2015, baada ya kuwaondoa wenyeji, Guinea ya Ikweta katika changamoto ya mikwaju ya penalti 4-2, baada ya mchezo huo kumalizika suluhu.
Michuano hiyo itahitimishwa rasmi kesho wakati Ivory Coast itakapomenyana na Ghana katika Dimba la Bata nchini Guinea ya Ikweta, ambapo michuano hiyo imeandaliwa.
Wakali wa bolingo wamejipatia nafasi hiyo baada ya kufanya kweli katika mikwaju ya penalti ambapo walipata yote na wapinzani wao wakiambulia miwili, huku mlinda mlango na nahodha Robert Kidiaba akiokoa mkwaju mmoja kati ya hiyo.
Mikwaju ya DR Congo ilifungwa na Cedrick Mabwati, Lema Mabidi, Chancel Mbemba na Gabriel Zakuani, wakati wa wenyeji Guinea Ikweta yaliwekwa kiamiani na Ellong Doulla na Juvenal Owono, huku Raul Bosio mkwaju wake ukimezwa na Kidiaba, wakati Javier Balboa uliota mbawa.

The Hero.... Kidiaba alipangua moja ya mikwaju ya Guinea Ikweta.


Hata hivyo, katika mchezo huo Guinea Ikweta walionekana kutokuwa na hamasa, ikiwa ni siku chache  tangu mashabiki wao wafanya vurugu uwanjani baada ya kichapo takatifu cha mabao 3-1 walichopokea kutoka kwa Ghana katika mchezo wa nusu fainali. Wakati Ivory Coast, wao walitinga fainali baada ya kuwavuruga DR Congo kwa mabao 3-0.
Uzalendo haswa...mashabiki wa DR Congo



No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...