Wednesday, January 30, 2013

MR BLUE ATOLEWA VYOMBO NJE


MSANII wa Muziki wa Kizazi  Kipya Bongo, Mr Blue anadaiwa kutupiwa vitu vyake vya ndani  leo mchana nyumbani  kwake Posta jijini Dar es Salaam anakoishi na mjomba wake,
Chanzo cha habari hii kimeeleza kuwa,Mr Blue a.k.a Kabaisa  ametolewa vyombo vyake vyote vya ndani  na watu wa Shirika la nyumba la Taifa, baada ya kujilimbikizia vyumba viwili kwa njia ya udanganyifu bila malipo yoyote. HABARI ZAIDI TUNAENDELEA KUZIFUATILIA  HIVYO ENDELEA KUWA NASI KARIBU. CHANZO G5CLICK
viwili kwa njia ya udanganyifu bila malipo yoyote. BU.

JACK PATRICK NUSU AMTOE ROHO MTU

 Mrembo aliyenusulika kuuwa na kipigo cha chupa kutoka kwa Jack Patrick, akiwa katika pozi muda mfupi baada ya kushonwa nyuzi tatu.
STAA wa Bongo anayetesa kwenye mitindo, Jacqueline Patrick anakabiliwa na msala wa kumtwanga na chupa nusu kumuua mrembo anayejulikana kwa jina la Hafsa Sasya, Risasi Mchanganyiko linanashuka nayo.
Habari zilizopenyezwa na chanzo chetu kutoka eneo la tukio zinasema kwamba, ishu ilitokea usiku wa kuamkia Jumamosi ya Januari 26, mwaka huu ndani ya Ukumbi  wa Elements Lounge uliopo Masaki, Dar.
CHANZO KINATIRIRIKA
Huku sharti la kutotajwa jina lake gazetini likisisitizwa na chanzo hicho, kilisema: “Unajua yule dada (Hafsa) anasoma Kurasini na anaishi Kijitonyama, namfahamu vizuri sana. Walipokutana na Jack pale ukumbini palitokea kutokuelewana kidogo.

“Baada ya muda hali ikawa sawa, watu wakajua yamekwisa. Jack akaenda zake chooni, aliporudi alikuwa na chupa na kwenda kumpiga nayo Hafsa. Mabaunsa wakamwondoa Jack ukumbini na kumwingiza Hafsa kwenye gari lake kwa lengo la kumpeleka hospitalini. Kilichoendelea hapo sijui.”
PEKUPEKU ZA RISASI
Mwandishi wetu aliingia mzigoni rasmi na kuanza kuichimba kwa kina habari hiyo ambapo alipata uhakika wa kutokea kwa tukio hilo na Jack kufikishwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay ambapo alifunguliwa kesi yenye jalada namba  OB/RB/1678/13  KUJERUHI.
Baada ya kujiridhisha kwa hilo, zoezi lililofuata lilikuwa ni kuwatafuta wawili hao ili waeleze wanachokijua kuhusu tukio hilo. Wa kwanza kupatikana alikuwa ni Jack.
BOFYA HAPA KUMSIKILIZA JACK
“Ni kweli kulitokea ugomvi siku ile...na ni kweli nilihojiwa na Polisi wa Kituo cha Oysterbay, lakini nimetoka kwa dhamana na kesi imekwenda mahakamani.”
HUYU HAPA HAFSA
“Mimi na Jack tulikuwa marafiki lakini nashangaa amenipiga na chupa bila sababu. Nimeshonwa nyuzi tatu. Siku ile alinikuta nimesimama na rafiki yangu mara akanipiga kikumbo kisha akaenda chooni, aliporudi akanikumba tena, nilipomuuliza ikawa kosa; akanipiga na chupa.

“Imeniuma sana maana amenipa jeraha usoni mwangu bila sababu ya msingi, maana sina ugomvi naye. Kwa sababu hili suala lipo mikononi mwa sheria, naamini itachukua mkondo wake.”

Mrembo anayekwenda kwa jina la Hafsa akiwa katika hali mbaya muda mfupi baada ya kushushiwa kipigo kikali na Jack Patrick

Tuesday, January 29, 2013

HATIMAYE LULU AACHIWA HURU KWA DHAMANA

 
Lulu akishuka katika gari la polisi baada ya kuwasili mahakamani leo.
 
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo imemwachia kwa dhamana msanii wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu' aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya kumuua msanii mwenzake wa filamu Steven Kanumba Aprili 7, 2012 bila kukusudia baada ya kukamilisha taratibu zote za dhamana.
Lulu akiingia katika chumba cha msajili wa mahakama ili kukamilisha dhamana yake.

Kutoka kushoto ni mama mzazi wa Lulu Lucresia Karugila, wakili wa Lulu bwana Kibatala na Dk. Cheni wakijadili jambo wakati wakisubiri dhamana ya Lulu.

Lulu (katikati) akitoka eneo la mahakama baada ya kukamilisha dhamana yake.

Lulu akiongea na wanahabari (hawapo pichani) baada ya kupata dhamana leo.

Lulu akiwa ndani ya gari baada ya kukamilisha dhamana yake.

Gari lililombeba Lulu likiondoka mahakamani.





Thursday, January 24, 2013

Tanzania ya pongezwa kwa kutatua migogoro Afrika


Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda akiwasili leo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kupokelewa na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini humo Bwana Hemed Mgaza (katikati) Kushoto ni Mwenyekiti wa Bunge na Makanu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Musa Azzan Zungu (Mb). Kulia ni Mhe. Sadifa Juma Khamis, (Mb).Mhe. Spika ameongoza ujumbe wa Wabunge watano kuhudhuria Mkutano wa tatu wa Kimataifa wa Jukwaa la Kibunge la nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu.


Spika Makinda na Spika wa Kenya Mhe. Kenneth Marende (kulia) wakiingia kwanye mkutano huo.

Ufunguzi wa mkutano wa Tatu wa PF –ICGLR (Forum of Parliaments of International Conference on Great Lakes Region – FP/ICGLR) mjini Kinshasa.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.

Picha ya pamoja ya maspika, Sekretarieti pamoja washirika wa maendeleo wa FP-ICGLR.
Jukwaa la Mabunge ya Jumuiya ya Kimataifa ya nchi za Ukanda wa Maziwa Mkuu (FP-ICGLR) limeitaja Tanzania kuwa mfano wa kuigwa kwa juhudi inazozifanya kuleta amani barani Afrika.

Pongezii hizo zimetolewa leo na jumla ya nchi wa kumi na mbili zinazounda Jukwaa hilo kwenye mkutano wa tatu unaoendelea kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zimewataja Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoa na watanzania kama wapenda amani barani Afrika

Hii ni kutokana na viongozi hao kujitolea kusuluhisha migogoro ya DRC/Rwanda na kundi la M23, migogoro ya Afrika ya Kati, mgogoro wa Sudani na Sudani Kusini, mgogoro wa Kenya baada ya uchaguzi mkuu na mingine mingi. Pamoja na Tanzania, Afrika Kusini nay imepongezwa

. Bunge la Tanzania limewakilishwa na Spika wa Bunge ambaye ameongoza ujumbe wa wabunge watano ambao ni Mhe. Mussa Azzan Zunge, Mhe. Pauline Gekul, na Mhe Sadifa Juma. Wengine ni Mhe. Mohamed Mbarouk na Mhe. Prudenciana Kikwembe.

RAIS KIKWETE AZURU MAKAO MAKUU YA FIFA


Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, akiwa katika picha ya Pamoja na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Joseph Sepp Blatter na Rais w Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF) Leodegar Chilla Tenga (kulia) wakati Rais Kikwete na ujumbe wake walip0tembelea Makao Makuu ya FIFA mjini Zurich,Switzerland Januari 23, 2013 kwa Mwaliko maalum wa FIFA.

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, akimweleza jambo Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Joseph Sepp Blatter (kulia) kuhusiana na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodeger Chilla Tenga. Tenga ambaye pia ni Mwenyeketi wa Baraza la Vyama vya Soka vya Afrika Mashariki (CECAFA).

Rais wa FIFA Joseph Sepp Blatter akimkabidhi Rais Jakaya Kikwete bendera maalum ya FIFA.

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Joseph Sepp Blatter wakiwa katika mazungumzo wakati Rais Kikwete na Ujumbe wake walipo walip0tembelea Makao Makuu ya FIFA mjini Zurich,Switzerland Januari 23, 2013 kwa Mwaliko maalum wa FIFA.

RAIS WA ZANZIBAR DK. MOHAMED SHEIN AKUTANA NA BALOZI WA MAREKANI NCHINI TANZANIA, ALFONSO LENHARDT IKULU MJINI ZANZIBAR

DIAMOND ALINASA PENZI LA PENNY WA DTV....NI BAADA YA WEMA, JOKATE,AVRIL NA WENGINE KIBAO


 
Hauwezi kupita mwezi bila kuibuka kitu kitakachomfanya aandikwe tena na tena. 
Katika picha iliyowekwa kwenye ukurasa wa Facebook wa msichana aitwaye Skyner Ally kuna picha inayomuonesha Diamond akiwa amelala usingizi wa pono na msichana anayedaiwa kuwa ni mtangazaji wa DTV, Penny Mungilwa aka Vj Penny.

Picha hii inajieleza yenyewe kwa pozi walilolaa kuwa ni wapenzi ama ni one night stand?
Hata hivyo tulipowasiliana na Penny alisema hiyo ni picha iliyopigwa walipokuwa kwenye scene ya movie wanayoigiza pamoja ambayo amesema hana uhakika lini itatoka!

Penny na Diamond ndani ya movie?????...!!? Ngoja tuisubiri hiyo movie

MKE WA MTU AMWAGA RADHI HADHARANI!


KITUKO cha aina yake kimejiri Jumamosi iliyopita ndani ya Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar wakati Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’ ilipokuwa ikitumbuiza

Katika onesho hilo, mwanamke mmoja anayedaiwa kuwa ni mke wa mtu alifanya kitendo cha aibu baada ya kusaula nguo zake zote na kubakia na nguo za ndani.

Katika onesho hilo, Extra Bongo ilikuwa ikiwashindanisha mashabiki wake kucheza staili yao ya Kizigo na washindi kujinyakulia zawadi za fedha.

Wakati bendi hiyo inayoongozwa na ‘Kamarade’ Ally Choki ikitoa burudani, ghafla mwanamke huyo alivamia jukwaa na kuanza kucheza kwa staili aliyokuwa akiijua mwenyewe.



Mpigapicha  alipojaribu kumpiga picha dada huyo alihamaki na kumjia juu huku kumtishia kumvunjia kamera yake huku akidai kuwa yeye ni mke wa mtu, hivyo hapaswi kupigwa picha.

“Mimi ni mke wa mtu ukifanya mchezo nitakutolea laana,” alisema mwanamke huyo huku akizishika nguo zake na kuanza kuzitoa mwilini mwake moja baada ya nyingine.

Wakati mwanamke huyo akiendelea na zoezi lake la kusaula nguo, alijitokeza dada mwingine ambaye aliambatana naye pamoja ukumbini hapo na kumwita kwa jina la wifi.

“Wifiii…, wifiii…, weee wifii pombe gani hizo, usivue nguo, usifanye hivyo ni aibu, itakuwaje kaka akiziona hizo picha magazetini?” alisema dada huyo aliyedaiwa kuwa ni wifi mtu lakini pamoja na kumpigia kelele hizo haikusaidia kumzuia mwanamke huyo mcharuko kusaula nguo zake.

Baada ya kuombwa sana na wifi yake, mwanamke huyo alivaa nguo zake na kuendelea na burudani hadi mwisho.

Haikufahamika mara moja kama mwanamke huyo alifanya kitendo hicho kutokana na pombe au hasira za kupigwa picha

WANANCHI WACHOMA NYUMBA ZA ASKARI POLISI MKOANI PWANI


KUNDI la wananchi wanaodaiwa kuwa na hasira, wamevamia kituo cha Polisi cha Kibiti Wilayani Rufiji na kufanya vurugu kubwa baada ya raia mmoja kufa kwa kile kilichodaiwa kipigo cha Polisi.

Chanzo chetu cha Habari kutoka Kibiti kinaipasha kuwa kijana aliyefariki kutokana na kipigo hicho ni Hamis Mpondi, ambaye mauti yamemfika wakati akipatiwa matibabu Hospitali ya Muhimbili.

Habari zaidi zinapasha kuwa hivi sasa wananchi hao wanaendelea kuteketeza nyumba za Askari Polisi hao zilizopo jirani na kituo hicho, licha ya Polisi kuendelea kufanya juhudi za kuwatawanya kwa mabomu katika eneo hilo.

Aidha wananchi hao wameanza kufunga barabara kuu ya Kilwa iendayo Mikoa ya Kusini, Lindi na Mtwara kwa mawe, magogo na kuchoma matairi ikiwa ni umbali wa kama kilometa moja kutoka kituo cha Polisi Kibiti.

Hali inaelezwa kuwa inazidi kuwa tete huku Polisi wa Kibiti wakiendelea na jitihada za kudhibiti hali hiyo kwa kufyatua mabomu hewani kujaribu kutawanya umati huo wa watu. Vurugu zinaendelea

Wednesday, January 23, 2013

CCM KIRUMBA HAPATOSHI LEO, NI YANGA DHIDI YA BLACK LEOPARDS YA AFRIKA KUSINI‏

Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga, Ernest Brandts amesema timu yake itafanya vizuri katika mechi ya marudiano ya kirafiki dhidi ya Black Leopards ya Afrika Kusini niliyopangwa kufanyika mapema jioni ya leo ndani ya uwanja wa CCM-Kirumba mjini Mwanza.
Brandts alisema wachezaji wake wote wamefikia kiwango kile anachotaka na mchezo huo utakuwa muhimu sana kwake kwani ni wa mwisho kabla ya kuingia katika kampeni za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Alisema kuwa Black Leopards ni timu nzuri na walipata mazoezi mazuri katika mechi ya kwanza iliyofanyika kwenye uwanja waTaifa jijini na kushinda kwa mabao 3-2.
“Ni mechi nzuri ambayo nadhani itakuwa ni kipimo kikubwa kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, wachezaji wangu wana viwango vizuri sana kwa sasa na naamini makosa yaliyofanyika katika mechi ya kwanza hawatayafanya tena,” alisema Brandts.
Msemaji wa Klabu Yanga, Baraka Kizuguto alisema jana kuwa pamoja na mechi hiyo kuwa ya maandalizi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara, pia wameamua kuicheza ili kuwapa burudani mashabiki wa Mwanza.
Kizuguto alisema kuwa Yanga haitakuwa na mechi yoyote katika mzunguko wa pili Kanda ya ziwa na hiyo ndiyo nafasi yao ya kuwaonesha uwezo wao mkubwa mashabiki wa Mwanza nini wamekipata kutoka Uturuki.
“Tuna mashabiki wengi sana Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla, hii ni fursa kwetu kwani mahsbaiki na wanachama watapata fursa ya kuona kiwango na maandalizi ya timu yao kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili,” alisema Kizuguto.


PETER OKOYE WA P SQUARE APATA MTOTO WA PILI



Wa katikati kwenye hii picha ndio mwimbaji Peter Okoye wa kundi la P Square kutoka Nigeria ambae mpenzi wake ambae bado hawajafunga ndoa kajifungua mtoto wao wa pili akiwa ni wa kike, wa kwanza ni wa kiume anaitwa Cameron na ana umri wa miaka minne.


Mpenzi wa Peter Okoye aitwae Lola Omotayo akiwa kitandani muda mfupi tu baada ya kujifungua, watoto wao wote wawili wamezaliwa nchini Marekani.

Peter Okoye akiwa Marekani january 2013 siku chache kabla ya mke wake kujifungua.

Lola akiwa na mtoto wao wa kwanza wa kiume, (Cameron).

WEMA SEPETU ANUNUA GARI INAYOKISIWA KUWA NA GHARAMA YA MIL.70 NA ZAIDI



Picha za Gari mpya ya Wema Sepetu aina ya Audi Q7 yenye rangi nyeusi zimeonekana kwenye akaunti ya Wema ya Instagram alipokuwa beach hivi karibuni na kuiandikia caption, ‘my baby at da beach.’

Kwenye akaunti ya meneja wake Martin Kadinda pia kuna picha nyingine ya gari hiyo aliyoiandikia maneno, ‘#maisha sio manhattan…..You can creat your own Manhattan in Tz… Hata kama ni Ya muda mfupi… #Kiphating.’

Gharama ya gari hiyo inaweza kuanzia shilingi milioni 70 na kuendelea.

JUX NDANI YA PENZI ZITO NA MKE WA MTU, JACKIE CLIFF







Unamkumbuka Jux? Yule chorus Killa wa kundi la Wakacha wazee wa Coders? Yeah, jamaa yuko kimya kiaina lakini kwa mujibu wa picha zake za Instagram the boy is living large! Pamba kali (kama kawaida yake), trip za pipa za hapa na pale kwenda ughaibuni na mambo kibao.

Kikubwa zaidi the songbird is apparently dating one of the hottest models in Tanzania, Jackie Cliff. Kama humfahamu vizuri Jackie anaonekana kwenye video za nyimbo kadhaa za Bongo Flava zikiwemo Nataka Kulewa wa Diamond na She got a gwan wa Ngwair!

Kupitia akaunti ya Instagram Jackie amepost picha akiwa na Jux na kuandika, “Dinner date with @juma_jux in Garden hotel.”

Na pia Jux kwenye akaunti yake amepost picha ya Jackie akijaribisha kuvaa viatu vyake (Jux) na kuandika, “baby tryn them #me Jordans…#dope though.”

"SINTAH AIFUNGUKIA BONGO MOVIE KUHUSU UKIMWI NA MAGONJWA YA ZINAA


MSANII mwenye maneno ya shombo kwenye tasnia ya maigizo Sintah, amefunguka kuwa anaiombea tasnia hiyo isikumbwe na dudu baya kama HIV na magonjwa ya zinaa, kutokana na tabia iliyopo ndani ya tasnia hiyo ya kuibiana wapenzi na kutoka wenyewe kwa wenyewe.

Kauli ya msanii huyo imekuja ili kuwafungulia mwaka vizuri na uwe wa mafanikio, ambapo alisema kuwa endapo wasanii hao wataendelea na tabia hizo basi kuna madhara makubwa yanaweza kutokea kwani baadhi ya wasanii wanafanya biashara chafu ya kutembea na wanaume wengi kwa lengo la kuendesha maisha.

Alisema kuwa hana nia mbaya na mtu yeyote na hayo ni mawazo ambayo yanaweza kuleta mapinduzi kwa tasnia hiyo ambayo imekuwa ikipewa sifa mbaya kila kukicha.

“Naipenda sana tasnia hii lakini nachukizwa na baadhi ya wasanii ambao hufanya mchezo wa kubadilisha wapenzi kama nguo, na matukio mengi machafu hufanywa na wasanii hasa pale wanapokuwa kwenye bonanza pengine mkoani au kambini,” alidai.

Hata hivyo aliongeza kuwa wapo wasanii wengine ambao hufanya kazi vizuri na hawajishungulishi na ujinga wowote lakini kuna makundi mengine ambayo yapo kwa ajili ya ngono na kuwapotosha wengine.

Tuesday, January 22, 2013

"MWAKA HUU JACK WOLPER HANA BWANA WA KUMCHUNA".....RAFIKI YAKE AVUJISHA SIRI


Msanii wa filamu bongo, Jackline Wolper, ambaye inadaiwa kuwa ndiye anayewafunika mademu wenzake kwenye tasnia hiyo kwa kumiliki mshiko mrefu, inadaiwa kuwa amekuwa akiwaza ndani ya mwaka huu atampataje bwana wa kumuhonga vitu vya kifahari kama bahati ilivyomdondokea msimu uliopita kutoka kijana mtafutaji Dallas.

Kuvuja kwa siri hii kumekuja siku chache baada ya mwandishi wa dt kufanya mazungumzo na baadhi ya wapambe wa msanii huyo, ambapo mmoja wao alidai kuwa msanii huyo kwa sasa hana mwanaume anayeweza kumpa vitu ya kifahari kama ilivyokuwa msimu uliopita, hata zile misheshe za kutoka hapa na pale zimepungua kutokana na hilo.

“Rafiki yangu bado hajapata mtu bwana najua ungeona kelele za mjini, saivi yupo tu kama hivi hamna mpya” kilidai chanzo.

Pamoja na ishu hiyo kuvuja Wolper aligoma kuzungumzia ishu hii badala yake alidai kuwa hakuna mtu anayejua siri zake na kama kuna mtu anajua basi abaki na hizo alizonazo.

CHADEMA WAIBEZA KAULI YA NAPE



Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, kimesema kuwa kauli iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM, NAPE NNAUYE, kuwa chama hicho kitakufa kutokana na kuwa na Sumu ya Ubaguzi, haina ukweli wowote, na kumtaka kiongozi huyo kutafakari zaidi kauli hiyo kwa maslahi ya Chama chake.

Mkurugenzi wa Sera na Mafunzo wa CHADEMA, BENSON KIGAILA, amesema CHADEMA hakiwezi kufa kwa dhana iliyozungumzwa na NAPE, na badala yake Chama hicho Tawala ndicho kinachoweza kufa kutokana na kukabiliwa, na changamoto nyingi ikiwemo ufisadi.

Katika Hatua nyingine CHADEMA kimemtaka Naibu Katibu wa CCM, MWIGULU NCHEMBA, kutoa ushahidi wa kauli aliyoitoa hivi karibuni, kuwa Chama hicho kimekuwa kikipanga mipango ya mauaji na kubainisha kuwa kauli hiyo, imelenga kulidhalilisha jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa

ASKARI WA JWTZ AKAMATWA NA PEMBE ZA NDOVU


 
JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limesema kwamba mwanajeshi aliyekamatwa juzi katika tukio la ujangili mkoani Arusha ni askari wake. Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe jana alimtaja askari huyo kuwa ni mwenye namba MT 59509 Sajenti, Azizi Athuman Yusufu ambaye alisema ni askari wa jeshi hilo na alikuwa dereva wa mkufunzi wa kijeshi kutoka Zimbabwe anayefundisha hapa nchini.


Hata hivyo Kanali Mgawe alisema mkufunzi huyo wa kijeshi, hakuwapo wakati wa tukio hilo. “Kweli huyo ni askari wetu. Alikuwa anamwendesha mkufunzi wa kijeshi kutoka Zimbabwe. Siku hiyo alimrudisha nyumbani kwake saa saba mchana na kwenda kupaki gari. Lakini baadaye saa moja usiku, alikwenda kulichukua gari hilo na kutokomea nalo kusikojulikana hadi alipokutwa katika tukio hilo,” alisema Kanali Mgawe.

Wakati JWTZ likitoa taarifa hiyo, Polisi mkoani Arusha jana lilieleza jinsi askari huyo alivyokamatwa. Hata hivyo namba ya askari huyo ilitofautiana na namba ya askari ikimtaja kuwa ni mwenye namba MT 59503.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema askari huyo alikamatwa saa 5:00 usiku wa Januari 20 mwaka huu. Alikutwa na pembe mbili za ndovu na bunduki moja aina ya Riffle yenye namba 458.

“Tunaamini bunduki hiyo ndiyo iliyotumika kwenye uwindaji huo haramu,” alisema.

Kamanda Sabas alidai kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa na wenzake zaidi ya wawili ambao walikimbia wakati mwenzao huyo anakamatwa eneo la Manyara Kibaoni Wilaya ya Karatu mkoani Arusha.

“Gari lililohusika kwenye uhalifu huu limethibitika kuwa ni mali ya JWTZ na uchunguzi unaendelea kujua namna gani wahusika walifanikiwa kuondoka nalo kambini na kwenda kulitumia kwenye uhalifu huo,” alisema Sabas.

Awali, habari kutoka eneo la tukio zimeeleza kuwa gari hilo lilikuwa na zaidi ya abiria watatu ambao mara baada ya matairi mawili kupasuka, moja la mbele kulia na jingine la nyuma kushoto watu wawili waliteremka na kutokomea porini na mizigo isiyojulikana.

Ilidaiwa kuwa baada ya wananchi kufika kwa nia ya kutoa msaada kwa majeruhi, mtuhumiwa aliyekutwa akiwa amevaa jaketi la JWTZ na suruali ya jinsi pamoja na bunduki, aliwahakikishia wananchi waliotaka kuwakimbiza watu hao wakidhani wamemwibia wasishughulike nao kwa kuwa hajaibiwa chochote.

Baada ya wananchi na askari wa jeshi la polisi waliofika kumtilia shaka mtuhumiwa, msako ulifanyika kuelekea walikokimbilia abiria hao garini na mizigo, lakini hawakuonekana.

MAONI YA MH. LOWASSA KWA TUME YA KATIBA MPYA



Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiongozana na Katibu Mkuu Mstaafu wa uliokuwa Umoja wa Nchi huru za Kiafrika (OAU),Dr. Salim Ahmed Salim ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, mara baada ya Mh. Lowassa kutoa maonai yake mbele ya tume hiyo.



Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa kukusanya Maoni ya Katiba mpya,mara baada ya kutoa maoni yake.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akipongezwa na Mjumbe wa Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba mpya,Dk. Senkondo Mvungi mara baada ya kutoa Maoni yake.

*YAFUATAYO NI SEHEMU YA MAONI ALIYOYATOA MH. EDWARD LOWASAA:
Kwanza ningependa kukupongeza wewe mwenyekiti Mh Jaji Warioba pamoja na tume nzima kwa imani kubwa ambayo Rais ameionesha kwenu, ni kwa kuwapa jukumu hilo zito na muhimu kwa nchi yetu.

Wananchi pia wamekuwa na imani kubwa na wamejenga matumaini ya kila kitu kwa tume hii. Kutokana na hilo wamekuwa wakitoa maoni ambayo mengine hayahusiani na katiba, yaani siyo ya kikatiba.Pengine na mimi nitakuwa miongoni mwao, kwa hiyo naomba radhi mapema, iwapo maoni yangu haya mengine , yataonekana si ya kikatiba.

Katiba yetu ya sasa ni nzuri, imetuongoza katika umoja na mshikamano wa kitaifa kwa muda wote huo.Lakini, kutokana na hali ya dunia ya sasa, ni vyema kuwepo na katiba mpya ili kuendana na hali halisi.

Kuna mambo manne ambayo kwa imani na mtizamo wangu ningependa yawemo katika katiba yetu ijayo.

1.ELIMU BURE

Moja ya haki za mtoto ni kupata elimu. Ningependa suala la elimu bure ya sekondari liwemo kwenye katiba yetu. Katiba itamke wazi kuwa elimu ya sekondari ni bure.Nchi yetu bado ina idadi kubwa ya watu wake ambao ni masikini.

Uwezo wao wa kipato ni mdogo.Naamini kabisa hili linawezekana na serikali inaweza kugharimia elimu ya sekondari ikawa bure. Hii itatoa nafasi ya kujenga taifa lijalo lenye idadi kubwa ya vijana watakaokuwa wamepata elimu ya sekondari.Wabunge wenzangu bila shaka wanalijua hili.

Ukweli katika majimbo yetu wazazi wamekuwa wakishindwa kulipia karo ya shule kwa watoto wao. Wabunge tumekuwa tukibeba mzigo huo japo kidogo. Kwa hiyo, kifungu cha ELIMU BURE KWA SEKONDARI, kiwepo kwenye katiba.

2.ADHABU YA KIFO-DEATH PENALT
Katiba ya sasa haisemi wazi kuhusu adhabu ya kifo.Inazungumzia tu haki ya uhai.Ibara ya 14 ya katiba hii ya jamuhuri ya muungano wa tanzania ya mwaka 1977 inatamka kiujumla tu kuwa KILA MTU ANA HAKI YA KUISHI NA UHAI WAKE KULINDWA.

Lakini , haki hiyo inanyang'anywa na kifungu nambari 196 cha sheria ya kanuni za adhabu sura ya 16(penal code ,cap 16), kinachotamka kuwa adhabu ya kifo(death penalty or capital punishment) kwa kosa la mauaji ya kukusudia.

Adhabu hiyo hiyo pia utolewa kwa kosa la uhaini.Sasa mapendekezo yangu mimi ni kwamba kuwe na ibara katika katiba mpya inayotamka wazi kuwa HAKUTAKUWA NA ADHABU YA KIFO HAPA NCHINI HATA KWA KOSA LA KUKUSUDIA AU UHAINI.

3.MATUMIZI YA FEDHA KATIKA UCHAGUZI
Katika sehemu nyingi hapa nchini mwananchi kama hana fedha hawezi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.Katiba mpya iwe na ibara inayofafanua ni kiasi gani cha fedha ambacho mgombea anaruhusiwa kutumia katika kampeni.Iainishe ni matumizi gani ya lazima ambayo mgombea hawezi kukwepa kutumia fedha katika kampeni zake, mfano kuwakusanya wapiga kura kwenda kupiga kura gharama hizo nani azibebe.

Katiba ifafanue rushwa ni nini kwenye chaguzi hizi.Au tuwe na mfumo wa PROPORTIONAL REPRESENTATION ,vyama viwe ndiyo vinaingia kwenye chaguzi kuwania majimbo na siyo wanachama,huko kila mtu atakuwa anapigania chama chake kupata kura nyingi ili wapate viti vingi zaidi, pengine hii itasaidia kuondoa kikwazo cha mtu kuwa na uwezo wa kifedha ndiyo aweze kuwania uongozi.


4.ARDHI

Kwa mwanadamu, kunyang'anywa haki ya kutumia ardhi ya nchi aliyozaliwa ni sawa na kunyanng'anywa haki ya uraia wake. Katiba hii ya sasa inawapa nguvu wakulima katika suala la ardhi, na kuwasahau wafugaji.

Wafugaji wamekuwa wakimbizi katika nchi yao, wamekuwa wakitangatanga kutafuta malisho ya mifugo yao, ile ardhi waliyokuwa wanaimiliki wakiondoka kutafuta malisho huku nyuma imekuwa ikimilikishwa watu wengine, wakulima au wawekezaji, hili kwakweli si jambo jema .

Tumeshuhudia migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji.Kwa hiyo, mimi ningependa katiba hii mpya impe mfugaji haki katika suala la ardhi kama.Ardhi ya wafugaji ilindwe, ifafanuliwe kikatiba haki yao hiyo. Kuwe na hali ya 50,50 situation kati ya mfugaji na mkulima katika suala zima la umiliki wa ardhi,kikatiba!

BAADA YA SINTAH KUMCHANA RAYUU KUWA YY NI KUNGURU ASIYEFUGIKA.......RAYUU NAE AJIBU MASHAMBULIZI KWA MATUSI MAZITO!


Rayuu
 
Ugomvi kati ya wasanii wa kibongo maarufu kama sintah na Rayuu umechukua sura mpya baada ya wasanii hao kuanza kuumbuana kwa maneno machafu.....

Kisa kilianza mwaka jana baada ya Rayuu kusambaza picha zake za nusu utupu, hali iliyomkera sintah na kuamua kumponda.......

Rayuu hakuishia hapo, mwaka huu kakianika tena kiuno chake huku nguo zake za ndani zikiwa njenje.....Sintah alifunguka tena na kumuita "KUNGURU ASIYEFUGIKA"....

Baada ya Rayuu kuitwa "kunguru", yeye amemuita mwenzie "Gubegube lililoshindikana tz"......

Haya ndo mabishano yao



HIKI NDICHO ALICHO KIANDIKA SINTA MTANDAONI JUU YA RAYUU

"SIKUENDA UINGEREZA KUUZA SURA.." IRENE WOYA



MSANII mahiri wa filamu Irene Uwoya, ameamua kuweka wazi kuwa safari yake aliyowahi kuifanya ya nchini Uingereza mwaka jana kwa ajili ya mazungumzo ya kufanya filamu ya kimataifa bado hayajazaa na matunda na hadi sasa wapo kwenye mazungumzo.

Kauli ya msanii huyo ilimfanya mwandishi wetu amdadisi zaidi, ambapo alisema kuwa kwa sasa kitu wanachokizungumzia ni namna watakavyoandika story ingawa hakutaka kuweka wazi ni story ya namna gani.

Hata hivyo alisema kuwa bado hawajafikia mazungumzo ya kulipwa kiasi gani na lini watafanya lakini anaamini kila kitu kitakuwa safi kwani watu hao wameonesha nia ya kufanya nae kazi.

Pamoja na hayo alishindwa kuwaweka wazi watu hao hata kwa kuwataja majina, kwa madai kuwa kwa sasa siyo wakati wake kwani muda ukifika mashabiki wake watajua anaenda kufanya kazi na kampuni gani.

“Bado tunaendelea na mazungumzo.Sikuenda huko kuuza sura .Najua watu wanasubiri kuona ukweli juu ya maneno yangu haya lakini nachotaka kusema ni kwamba ni kweli nilienda kwa ajili ya mazungumzo ila bado mambo hayajakaa sawa,” alisema Uwoya

LULU KUOMBA DHAMANA MAHAKAMA KUU IJUMAA HII

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Januari 25 mwaka huu, itasikiliza ombi la kupatiwa dhamana ya msanii wa Filamu Bongo, Elizabeth Michael  'Lulu' ambaye anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia  kwenye mahakama hiyo  kesi yenye Na. 125/2012 mauaji ya  msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Ombi hilo la dhamana ambalo tayari litasikilizwa na  Jaji Zainabu Mruke limewasilishwa mahakamani hapo na mawakili wake.


Monday, January 21, 2013

YALIYOJIRI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA YANGA JANA, SENDEU, MWESIGWA WAFUTIWA UANACHAMA

 Baadhi ya wanachama wa Klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, kutoka maeneo mbalimbali, wakitawanyika nje ya ukumbi wa bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay jana mchana mara baada ya kumalizika kwa mkutano mkuu wa Mwaka, ambao umefanikiwa na kuweza kufanya mabadiliko katika baadhi ya maeneo ya nafasi za uongozi, ambapo aliyekuwa Ofisa Habari wake, Louis Sendeu na aliyekuwa Katibu Mkuu, Selestine Mwesigwa, wamefutiwa Kadi zao za uanachama, kwa kile kilichoelezwa kuwa mwezi Septemba, mwaka jana walitinga Mahakamani kupinga kufukuzwa kazi katika Klabu hiyo.

Katika suala hilo la Kimahakama, Mwesigwa aliishitaki Klabu ya Yanga akiidai kiasi cha Sh. 183,400,050, huku Sendeu akidai kiasi cah Sh. 79, 900,050, ambapo Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji, aliwahoji wanachama, juu ya hilo na kupata jibu la pamoja kutoka kwa wanachama waliosema kwa pamoja kuwa, ''Wavuliwe uanachama kwa kukosa uzalendo na Klabu yao''.

Ndipo Manji alichukua jukumu la kutangaza kuvuliwa uanachama kwa watu hao na kusema kuwa wamewaongeza wajumbe wawili kwenye bodi ya Udhamini ya Klabu hiyo, ili kutimiza idadi ya watu saba, ambao ni Amir Kungwe na George Mkuchika.

Mkutano huo uliratibiwa na kampuni ya Prime Time Promotions Ltd ya jijini Dar na kurushwa Live kupitia Clouds TV, aidha Mkutano huo ulionekana kunoga zaidi baada ya timu hiyo ya Yanga jana yake kuonyesha makucha yake na vitu adimu ilivyorejea navyo kutokea nchini Uturuki kwa kuifunga timu ya Black Leopards ya nchini Afrika kusini katika mechi yao ya kimataifa ya kirafiki iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Taifa na kuibuka na ushindi wa mabao 3-2.

Mwenyekiti Mpya wa Club ya Yanga Africans, Yusuf Manji akifafanua baadhi ya mambo mbalimbali kwenye mkutano huo,uliochanganua mambo mbalimbali zikiwemo changamoto za timu hiyo, maendeleo ya Klabu hiyo pamoja na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha mpira maeneo ya Jangwani,jijini dar, Sahihisho la katiba yao, masuala mbalimbali yanayohusiana na wanachama wao, ustawi wa wanachama wao, mikataba baina yao na wadhamini wao na mambo mengine mengi yaliyoongelewa.

Sehemu ya meza kuu ya mkutano huo ilivyokuwa.

Makamu mwenyekiti wa timu ya Yanga,Clement Sanga akitolea ufafanuzi moja ya jambo lililoulizwa na wajumbe wa mkutano huo.

Beki mahiri wa Yanga, Shadrack Nsajigwa (kulia) akipeana mkono wa shukrani na Mwenyekiti wa Yanga,Yusuf Manji mara baada ya kutajwa kuwa ndiye mchezaji aliyedumu Yanga kwa muda mrefu miongoni mwa wachezaji waliopo hivi sasa, na kuwa mchezaji mwenye nidhamu zaidi, hivyo alizawadiwa barua ya shukurani na kitita cha shilingi milioni moja.




Pichani juu na chini ni baadhi ya Wajumbe wa timu ya Yanga waliopata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali kwa Kamati ya Utendaji,mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria mkutano huo.

Mwenyekiti wa Yanga,Yusuf Manji sambamba na Makamu mwenyekiti wa timu hiyo,Clement Sanga wakifatilia jambo kwa makini ukumbini humo.

Baadhi ya wachezaji wa timu ya Yanga pia walihudhuria mkutano huo uliohusu mikakati mbalimbali ya kuimarisha timu hiyo.

Baadhi ya Wazee wa baraza wa timu ya Yanga wakifautilia kwa makini yaliyokuwa yakijili kwenye mkutano huo mkuu wa Kihistoria.

Kocha mpya wa timu ya Yanga,kutoka nchini Uholanzi Ernest Brandts nae aliruhusiwa kutoa yake machache kuhusina na timu yake ya Yanga.


Baadhi ya Wanachama wa Yanga waliofurika kwa wingi ndani ya mkutano mkuu wa timu hiyo uliofanyika ndani ya bwalo la Maofisa wa Polisi,Oysterbay jijini Dar es salaam mapema leo asubuhi na kumalizika mapema jioni ya leo.

Msanii mahiri wa kizazi kipya, Barnaba, pamoja na wasanii wenzake kutoka THT wakitumbuiza kwenye mkutano huo.

Mtangazaji machachari wa kipindi cha michezo,Clouds FM/TV Mbwiga Mbwiguke, akiwaweka sawa wanachama wa Yanga waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wao mkuu wa Mwaka.

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...