Friday, January 6, 2012

CHARLES BABA, GOODBYE TWANGA PEPETA

Msanii wa Muziki wa Dansi nchini,Charles Gabriel a.k.a Charles Baba akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumzia nia yake wa kujitoa rasmi katika Bendi yake ya awali ya African Stars (Twanga Pepeta) kwenye mgahawa wa Hadee's uliopo katikati ya Jiji.Charles Baba pamoja na kutangaza nia yake hiyo,pia amemtangaza Meneja wake Mpya,Bw. Bernard Msekwa ambaye atasimamia shughuli zake zote za Kimuziki ikiwa ni pamoja na kuingia mikatana na Bendi yeyote itakayomuhitaji.
Meneja Mpya wa Msanii wa Muziki wa Dansi nchini,Charles Baba ,Bw. Bernard Msekwa akisisitiza Jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na msanii wake huyo leo kwenye mgahawa wa Hadd's uliopo katikati ya jiji la Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Waandishi wa habari waliofika kumsikiliza Msanii huyo pamoja na Meneja wake wakisikiliza kwa makini.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...